UDOM WAPONGEZWA MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA (SABASABA)


  • 9 months
  • Directorate of Research, Publications and Consultancy

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Prof. William Mwegoha, amepongeza uongozi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa kijipanga vyema katika kuhudumia wananchi kwenye maonesho ya 47 ya Kimataifa SABASABA.

Pongezi hizo amezitoa alipotembea banda la UDOM leo, na kuonyesha kufurahishwa na bunifu na tafiti zinazoonyeshwa katika banda la UDOM, na hasa ubunifu wa kudhibiti matumizi ya rasilimali maji. Aidha, amewapongeza Wafanyakazi na washiriki wote wa maonyesho hayo kwa namna walivyojipanga kutoa Huduma kwa Wananchi na kuwahimiza Wananchi kufika kwenye Banda hilo kujifunza zaidi kuhusu Huduma za Chuo Kikuu cha UDOM.

Comments
Send a Comment